Ajira Mpya Dereva Daraja II

Dereva Daraja II - Ajira 1 

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti anapenda kuwatangazia nafasi ya kazi kwa madereva wenye ufaulu na uzoefu wa udereva daraja la II.

Wajibu na Majukum

  • Kukagua gari kabla na baada ya safari ili kubaini hali ya usalama wa gari;
  • Kuwapeleka watumishi maeneo mbalimbali kwenye safari za kikazi;
  • Kufanya matengenezo madogo madogo ya gari;
  • Kukusanya na kusambaza nyaraka mbalimbali;
  • Kujaza na kutunza taarifa za safari zote katika daftari la safari;
  • Kufanya usafi wa gari; na
  • Kufanya kazi nyingine kadri atakavyoelekezwa na Msimamizi wake.

Elimu na Uzoefu:

  • Mwombaji awe na Cheti cha Kidato cha Nne (Form IV)
  • Awe na Leseni ya Daraja E au C ya uendeshaji magari ambayo amefanyia kazi kwa muda usiopungua mwaka mmoja bila kusababisha ajali. 
  • Awe amehudhuria mafunzo ya msingi ya Ufundi Stadi (VETA) au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.

Kima cha Mshahara: TGS B

💥Matangazo 🎄


*

Post a Comment (0)
Previous Post Next Post